BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAKAMU WA RAIS AJUMUIKA NA MAELFU YA WAUMINI WA DINI YA KIISLAM KATIKA SWALA YA EID EL FITR VIWANJA VYA MNAZI MMOJA DAR ES SALAAM


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal (katikati),Sheikh Mkuu,Issa Shaaban Simba,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadick na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Sheikh Mussa Salum wakijumuika na Waumini wengine wa Dini ya Kiislam kwenye Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam leo.CHANZO MTAA KWA MTAA BLOG


Sehemu ya Waumini wa Dini ya Kiislam wakiwa kwenye Ibada ya Eid el Fitr katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.


Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,Sheikh Mussa Salum akitoa Khotuba katika Idada ya Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam leo.

Mawaidha yakiendelea mara baada ya Swala ya Eid el Fitr.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa salamu za Eid el Fitr leo mara baada ya Swala iliyofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ulinzi,Dkt. Hussein Mwinyi (katikati) akijumuika pamoja na Waumini wenzake wa Kiislam katika Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam leo.

Masheikh mbali mbali wakiwa kwenye ibada hiyo.


Umati wa Waumini wa Kiislam ukiwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam leo,tayari kwa kushiriki ibada ya Eid El Fitr.


Wakinamama pia walijitokeza kwa wingi wao kwenye Ibada hiyo.

Watangazi wa TBC Taifa wakiongozwa na Maalim Sued Mwinyi wakirusha matangazo live.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohamed Gharib Bilal akipeana mkono wa Eid na baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislam mara baada ya Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja,Jijini Dar es Salaam leo.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: