BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MKURUGENZI WA MASHTAKA WA SERIKALI AWAFUTIA HATI YA MASHTAKA MAPROFESA NA WAHADHIRI SAKATA LA UTUPAJI WA VIUNGO VYA MAITI YA BINADAMU JALALA MAHAKAMANI.

Wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU) cha Dar es Salaam wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni jana. Picha na Salim Shao.

Dar es Salaam.
Sakata la kutupwa kwa viungo vya binadamu bila kufuata utaratibu jana liligeuka sinema wakati maofisa wanne wa Chuo Kikuu cha Tiba na Teknolojia (IMTU), walipofikishwa mahakamani Dar es Salaam.
Maofisa hao ambao ni maprofesa na wahadhiri wa chuo hicho walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kushindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu.


Baada ya mashtaka hayo kusomwa na taratibu za dhamana kukamilika huku mmoja wao akishindwa kutimiza masharti, watuhumiwa hao walirejeshwa kizimbani na kufutiwa mashtaka hayo kwa amri ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DDP) aliyewasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka hayo.


Hata hivyo, furaha waliyoipata washtakiwa hao, Venkat Subbaiah (57), Appm Shankar Rao (64), Prabhakar Rai (69) na Dinesh Kumar (27) ilikuwa ya muda tu, kwani polisi waliokuwapo mahakamani hapo waliwakamata tena na kuondoka nao.


Hati ya mashtaka


Akiwasomea mashtaka, Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Polisi, Magoma Mtani alidai kuwa washtakiwa hao Julai 2014 katika eneo la Mpigi Majohe, walishindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu waliyoitumia kufundishia wanafunzi wa udaktari kinyume na Kifungu cha 128 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya mwaka 2002.


Alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walishindwa kuandaa hati ya ofisa mchunguzi wa vifo vyenye mashtaka (coroner).


Baada ya kusomewa mashtaka hayo watuhumiwa wote waliyakana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.


Hakimu Mwandamizi wa mahakama hiyo, Kwey Rusemwa alitoa masharti ya dhamana akiwataka kila mmoja wao kuwa na wadhamini wawili ambao ni raia wa Tanzania na wanaofanya kazi kwenye taasisi zinazotambulika kisheria.


Washtakiwa watatu walikamilisha masharti hayo lakini mmoja alishindwa kutokana na kuwa na mdhamini ambaye si raia wa Tanzania.


Mashtaka yafutwa


Wakati washtakiwa hao wakikamilisha taratibu za dhamana wakiwa ndani ya mahakama hiyo, Wakili wa Serikali, Salum Ahmed aliingia na kuiomba mahakama kuifuta kesi hiyo chini ya Kifungu cha 91 (1) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA) kwa kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi yao.




Kifungu hicho cha sheria kinampa mamlaka DPP kuifuta kesi mahakamani wakati wowote pale anapoona hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi ya mtu yoyote.


Baada ya kuwasilishwa kwa ombi hilo, Hakimu Rusemwa aliwaachia huru washtakiwa hao bila masharti yoyote.


Wakamatwa tena


Muda mfupi baada ya washtakiwa hao kuwa huru, walianza kutoka mahakamani kwa furaha lakini kumbe furaha yenyewe ilikuwa inaishia mlangoni mwa mahakama hiyo tu kwani walikutana na polisi waliowakamata tena na kuwaweka chini ya ulinzi.


Wakati washtakiwa hao wakiwa chini ya ulinzi, Wakili wao, Gaudiosus Ishengoma alieleza kusikitishwa na kitendo hicho, akidai DPP aliwafutia mashtaka wateja wake na kuwaachia huru ili awafungulie mashtaka mengine ambayo hayana dhamana.


Baada ya washtakiwa hao kukamatwa upya walipandishwa katika gari aina ya Toyota Land Cruiser na Toyota RV4 na kurejeshwa polisi.


Akizungumzia kitendo hicho baadaye jana, DPP Eliezer Feleshi alisema kwa ufupi: “Kuna taarifa zilihitaji kufanyiwa kazi kwanza.”MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: