BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KOCHA MKUU WA KLABU YA SIMBA SC AACHA UNAFIKI WA UYANGA NA SIMBA, AMMWAGIA SIFA KEDEKEDE MSHAMBUALIAJI MPYA WA YANGA "JAJA".


Mshambuliaji wa Yanga, Genilson Santos ‘Jaja’ akijaribu kufunga katika mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii dhidi ya Azam, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Yanga ilishinda 3-0. Picha na Michael Matemanga.


Da r es Salaam.
Kocha wa Simba, Patrick Phiri amesema nyota wa Yanga, Genilson Santos ‘Jaja’ ni mshambuliaji hatari na mwenye akili nyingi anapofika golini.


Phiri alimshuhudia Jaja akifunga mabao mawili na kuiongoza Yanga kushinda 3-0 dhidi ya Azam katika mchezo wa Ngao ya Jamii.


Mzambia huyo, Phiri, alilimbia gazeti hili kuwa licha ya watu wengi kumbeza Jaja, lakini ni mshambuliaji hatari anapolikaribia lango na hapaswi kukabwa na mabeki legelege kwani wakati wowote anaweza kufunga.


Phiri alisema Jaja ana nguvu licha ya kutokuwa na kasi, lakini ana uamuzi mzuri anapokuwa karibu na lango, kitu ambacho washambuliaji wengi hawana.


“Ni mchezaji mzuri, nimependa anavyofanya uamuzi anapofika katika eneo la hatari, ana uamuzi wa haraka ambao wengi hawategemei, licha ya kuwa ni mzito, lakini ni hatari na anapaswa kuchungwa mno na mabeki.


Kikosi cha Phiri kitaivaa Yanga Oktoba 12, hivyo amewataka mabeki wake kuwa makini watakapocheza na Yanga, ambao safu yao ya ushambuliaji sasa itakuwa ikiongozwa na Jaja.


“Tunatakiwa kumuangalia sana siku tutakapokutana na Yanga, inabidi tumfungie kazi, nimependa jinsi alivyofunga lile bao la pili, washambuliaji wengi wasingeweza kufanya kile alichokifanya, anaonyesha ana akili,” alisema Phiri.


Jaja alipata wakati mgumu katika mchezo huo ulipoanza kiasi cha kufikia baadhi ya mashabiki wa Yanga kumpa presha kocha Marcio Maximo amtoe, lakini kocha huyo Mbrazil ni kama aliweka pamba masikioni huku akiamini mchezaji huyo atawanyamazisha.


Katika hatua nyingine, Maximo alisema alilazimika kutumia mifumo mitatu tofauti katika mchezo wao dhidi ya Azam.


“Nilianza na mfumo wa kukaba eneo la katikati nikimtumia Said Juma aliyemudu vema nafasi hiyo na baadae kumtoa na kumuingiza Hassan Dilunga naye alifanya kazi niliyomtuma ipasavyo,” alisema Maximo.


Kocha huyo aliongeza kuwa baada ya kuona wapinzani wao wamepoteana katikati ya uwanja aliwataka wachezaji wake kupiga mipira mirefu kwa kutumia kasi ya Mrisho Ngasa na Simon Msuva.


“Niliamua kumtoa Nizar (Khalfani) na kumuingiza Msuva, ambaye ana kasi na aliimudu nafasi yake pia kama ilivyokuwa kwa wengine walioingia,” alisema kocha huyo na kuongeza.


“Mfumo wa tatu nilioutumia kwenye mechi hii ni wa kuzuia ambapo niliamua kumtoa Jaja, Niyonzima (Haruna) na Ngassa (Mrisho) na kuwaingiza Omega Seme, Hussein Javu na Kiiza (Hamis).


“Nilijua fika baada Yanga kuongoza mabao mawili beki ya Azam itataka kupanda ili wasawazishe hivyo timu yao itacheza kwa mtindo wa kushambulia zaidi, nikaamua kuwaingiza Kiiza, Javu na Omega ili wakabe kote,” anasema.


Alisema aliisoma Azam na kubaini udhaifu wao hivyo akalazimika kutumia mfumo wa kukaba, mbio na kuzuia ambao umewasaidia kuwanyamazisha wapinzani wao.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: