BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHEZEA MISS TZ 2014 SITTA MTEMVU WEWE MBELE YA TAJI SUBUTU !!! UBISHI JUU YA UMRI HALISI WA MISS TANZANIA NDIYO HUU, KAMA KUDANGANYA BASI KAWADANGANYA WATANZANIA NA DUNIA KIDIGITAL.

Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu akizungumza machache na waandishi wa habari.
Mkurugenzi wa LINO International Agency ambao ni Waandaaji wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga hii leo amezungumza na waandishi wa habari juu ya sakata la umri halali wa Mrembo alietwaa taji hilo Mwaka huu, Sitti Abbas Mtemvu.

Lundenga amelitolea ufafanuzi suala la umri wa mrembo huyo kulingana na vilelezo alivyopewa na Sitto Abbas Mtemvu wakati akijiunga na mashindano hayo

"Katika mashindano yetu, Washiriki wote hujaza fomu maalum zilizoandaliwa na Kamati ya Miss Tanzania. Katika fomu alizojaza mrembo wa Miss Tanzania 2014 Sitti Abbas Mtemvu amejaza tarehe yake ya kuzaliwa ambayo ni Mei 31,1991 na hivyo kuwa ni sahihi kushiriki mashindano yetu" Alisema Lundenga mbele ya wanahabari hao.

Lundenga aliendelea kusema kuwa Mashindano ya Miss Tanzania hayaruhusu mshiriki yeyote mwenye mtoto kushiri,hivyo katika suala la Sitti Mtemvu kuwa ana mtoto,hilo kalina ukweli wowote bali ni uvumi tu wa kwenye mitandao ya kijamii baada ya Mrembo huyo kuonekana akiwa katika picha na mtoto alieomba kupiga nae.

Hata hivyo, maswali ya waandishi wa habari kwa Miss Tanzania yalizua utata mwingine baada ya kuonekana cheti kilichooneshwa kwa waandishi hao kimetengenezwa September mwaka huu.

Waandishi walihoji kuhusu cheti chake cha kuzaliwa cha awali ambacho alikitumia kupata passport na leseni ya udereva, mrembo huyo alisema cheti hicho kilipotea na alitoa taarifa polisi. Waandishi hao walipotaka kujua kituo cha polisi alichoripoti upotevu wa cheti hicho, alisema hataki kuzungumzia suala hilo.
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya sakata la umri halali wa Mrembo alietwaa taji hilo Mwaka huu, Sitti Abbas Mtemvu (kushoto),katika mkutano huo Lundenga alitolea ufafanuzi swala la umri wa Mrembo huyo kulingana na vilelezo alivyopewa na mrembo huyo wakati akijiunga na mashindano hayo
Nakala halisi ya Cheti hicho inayoonyesha Mrembo huyo amezaliwa Mei 31, 1991.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: