BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WATU WATIMUA MBIO OVYO KUMKIMBIA FISI ALIYEINGIA MJINI KISHA KATIKA MADUKA SINGIDA MCHANA KWEUPE.


Katika hali isiyo ya kawaida wakazi wa Manispaa ya Singida wameingiwa na taharuki na kuanza kukimbia ovyo baada fisi kuonekakana katikati ya mji wa singida akiwa anakimbia na kuingia katika maduka ya wafanya biashara. 

 
Wakieeleza kwa hisia tofauti baadhi ya wakazi huku wengine wakiwa wamepanda juu ya mapaa ya nyumba pamoja na watoto wao kwa hofu ya kuumwa,wamesema kuonekana kwa fisi mjini katikati ni jambo la ajabu kwani wanyama kama hao honekana vijiji au porini,wengine wamesema labda myama huyo amechelewa kurudi vichakani wakati alipokuwa amekuja kula mabaki ya chakula mjini.

Akielezea tukio hilo afisa maliasili mkoa wa singida Bwana Charles Kidua amesema pamoja na kwamba wanyama kama fisi wapo katika manispaa ya singida na pindi wanapo onekana katika maeneo ambayo siyo ya kawaida ,Basi wananchi watoe taarifa kwa mamlaka husika kwani wanyama kama haho wana weza kuwa na ugonjwa wa kichaa ,badala ya kujichukulia hatua mkononi ya kuwauwa.

Kutokana na umati wa wananchi kuwa wengi wakati wakimfukuza fisi huyo bila kujali askari waliokuwa wakituliza fujo huku wakiwa na silaha,wanachi walifanikiwa kuwapokonyo askari fisi baada ya kumtega na kamba huku wakiimba tunataka fisi wetu na kuamua kumkimbiza mjini huku wakimpiga umbali wa kilomita mbili.ITV
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: