BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

UNYWAJI WA MAZIWA HUZUIA MARADHI YA AKILI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbeT7TESP2BrONCNTDgPwWzmh1FYonsElEa1o6eDdNpgK_snfoMzbL3_jmtYoO4mij2Ly0-IhkxuhNGSeqKFleYCwVqW83ip0D8C_awj9hTsUgjygszegUvwtr00i9LEVCYdUClKEMrNOu/s400/Chef+Issa+yogurt+(2).jpg 

Maziwa huimarisha seli za ubongo

Wanasayansi wagundua chembechembe za glutathiona katika maziwa ambazo hulinda ubongo kuharibika



Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na wanasayansi kutoka nchini Marekani ni kwamba unywaji wa glasi 3 za mawiza kwa siku hulinda na kudumisha seli za ubongo wa binadamu.


Wanasayansi wamefahamisha kuwa, chembechembe za glutathiona zinazopatikana katika maziwa hulinda seli za ubongo na kusababisha maziwa kupunguza madhara yanayoweza kuukumba ubongo na kusabaisha akili kudhurika.


Chembechembe hizo hupunguza kasi ya ugojwa wa Alzheimer na Parkinson kumsibu binadamu.


Dr. Debra Sullivan, mmoja wa waanzilishi wa mradi kuhusu utafiti huo alisema kuwa, kwa muda mrefu tunafaham kuwa maziwa ni muhimu kwa mifupa na misuli ya binadamu ila kwa sasa tumegundua pia kuwa maziwa ni muhimu kwa ubongo.


Ili kufaanikisha utafiti huo, wanasayansi hao walifuatilia lishe ya bongo za watu wazima wenye afya njema na kugundua kuwa watu wanaokunywa kwa uchache glasi 3 za maziwa kwa siku walikutwa na idadi ya kuridhisha ya chembechembe za glutathiona.


Utafiti huo ulichapishwa katika gazeti la "American Journal of Clinical Nutrition".
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: