BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAFUASI 11 WA CUF WAVAMIWA NA KUJERUHIWA VIBAYA WAKATI WAKITOKA KATIKA MKUTANO VISIWANI ZANZIBAR.


Mbunge wa Mtambile (CUF), Masoud Abdallah Salim.
Wafuasi 11 wa Chama cha Wananchi (CUF) wamevamiwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana wakati wakitokea katika mkutano wa hadhara wa chama hicho.

Tukio hilo lilitokea juzi jioni eneo la Fuoni Jitimai, wakati wakirudi nyumbani baada ya mkutano huo, uliofanyika Makunduchi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja, Juma Sadi, alisema watu wasiojulikana waliwajeruhi wafuasi hao, ambao walikuwa katika gari na majeruhi hao kukimbizwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja na baadhi yao wamepewa ruhusa na wengine wamelazwa.

Kamanda Sadi alisema Jeshi la Polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kuwatia mbaroni waliohusika.

Wakati huo huo, Mbunge wa Mtambile (CUF), Masoud Abdallah Salim, jana alilitaka Bunge lijadili kwa dharura hali ya amani visiwani Zanzibar kwa maelezo kuwa wanachama wa CUF, wamepigwa na kujeruhiwa.

Alisema kupigwa kwa wafuasi na wanachama wa CUF kunahatarisha amani visiwani humo na Tanzania kwa ujumla hivyo, akaliomba Bunge lijadili hali hiyo. Akijibu mwongozo huo, Spika wa Bunge, Anne Makinda, alimtaka aandike hoja yake na aiwasilishe kwa Katibu wa Bunge kwa njia ya maandishi.
CHANZO: NIPASHE
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: