BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SERIKALI YAPOKEA LAWAMA KIBAO JUU YA KUSHINDWA KUWALINDA ALBINO.

http://ltastudent.lodiusd.net/Teodoras/Images/Albino%20child%20with%20black%20bro.jpg 

Kijana akiwa amembeba mdogo wake, Picha ya maktaba.

Serikali imelaumiwa kuwa imeshindwa kuweka mkazo katika kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kama inavyofanya kwa wanyama kama tembo hali inayosababisha mauaji ya watu hao kuendelea nchini.
Aidha, Serikali imelalamikiwa kwa kuzitengea fedha kidogo Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na Wizara ya Kazi na Ajira ambazo haziwezi kusaidia kutekeleza miradi ya maendeleo katika wizara hizo.
Mbunge wa Viti Maalum (CUF), Riziki Omari Juma, alisema mauaji ya albino yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara hali inayozua maswali kwa wananchi kuhusu mahali Taifa linapopelekwa.
Juma aliitaka serikali iweke utaratibu wa kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi badala ya kuendelea kufanya uchunguzi kusaka wahalifu kila unapotokea uhalifu.
“Kila siku matukio ya albino kukatwa viungo na wengine kuuawa yanatokea, lakini hatuoni serikali ikichukua hatua kuwalinda, tembo wanalindwa sana na ikitokea ameuawa mmoja tu wahalifu wanasakwa, lakini albino akiuawa hakuna hatua zinazochukuliwa,” alisema.
Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Maulidah Komu.
Juma aliitaka serikali kufuatia wafanyakazi wa ndani ambao wamekuwa wakinyanyaswa na mama na baba mwenye nyumba kwa kulipwa ujira kidogo.
Naye Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, alisema serikali ianzishe utaratibu wa kuanza kutoa mikopo kwa vijana wanaomaliza darasa la saba ili wapate fursa ya kujiunga na vyuo vya Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA).
“Vijana wanaomaliza darasa la saba wengi wanashindwa kupata nafasi ya kupata nafasi ya kujiunga na masomo VETA kwa kukosa pesa, hivyo ni wakati sasa kwa serikali ianze kuwakopesha mikopo kama inavyofanya kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu,” alisema.
Mbunge wa Mafinga (CCM), Mendrad Kigola, alisema tatizo la ajira kwa vijana limeendelea kuwa kubwa na sasa waliomaliza vyuo vikuu wanaamua kujiajiri katika kazi ya kuendesha pikipiki (bodaboda), hivyo serikali ianze kuwakopesha bodaboda.
Kigola alisema mashirika mengi ya umma yanalipa viwango vidogo vya mishahara na kutaka serikali ifuatilie hali hiyo kwani haiwezekani mashirika madogo ndiyo yalipe mishahara mikubwa na mashirika makubwa yanalipa kidogo.
Alisema Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto haijamsaidia mwanamke wa kijiji katika kupata haki zake za msingi na kusababisha aendelee kukabiliwa na umaskini wa kiwango kikubwa.
Kigola alisema Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Kazi Duniani (ILO) yasaidie katika kuwaletea maendeleo wanawake wa vijijini ambao wanakabiliwa na changamoto nyingi.
Naye Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Maulidah Komu, alisema watoto yatima na watoto wa mitaani serikali haijawasaidia, badala yake imekuwa na mikakati ya muda mrefu ambayo haiwasaidii walengwa.
“Watoto yatima na wa mitaani wanapata tabu sana mfano, kuna nyumba moja ya kuwalea ilikuwa Morogoro, walikuwa wanafanyiwa kitu kibaya serikali haichukui hatua,” alisema.
Komu alisema inashangaza baadhi ya wabunge licha ya kutambua kero zinazowakabili wananchi, lakini wanaunga mkono kwa asilimia 100 bajeti za wizara, lakini wanapochangia wanaanza kuorodhesha kero lukuki zilizopo katika majimbo yao.
CHANZO: NIPASHE
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: