BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAWAZIRI WATANO WA RAIS JAKAYA KIKWETE WADONDOKA KATIKA KURA YA MAONI NDANI YA CCM, YUMO CHIKAWE NA AMOSI MAKALLA.

Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiislamu
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiislamu Kondoa Dodoma, Hamisi Salum akikabidhi kadi ya CCM kwa ajili ya uhakiki wa taarifa zake kabla ya kupiga kura kumchagua mgombea udiwani na ubunge wa jimbo hilo katika Kituo cha Maji ya Shamba. Awali, kura za kituo hicho zilichomwa baada ya kubainika kuwa na udanganyifu. Picha na Shakila Nyerere 
 
Dar/mikoani. Kishindo cha kura za maoni ndani ya CCM kimeendelea kuwakumba baadhi ya vigogo wa chama hicho baada ya jana mawaziri wengine watano kuanguka.


Miongoni mwao ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe aliyekuwa akiwania kupitishwa tena kugombea tena ubunge wa Nachingwea.


Chikawe ambaye pia alishindwa katika kinyang’anyiro cha urais kupitia chama hicho, alidondoshwa na Hassan Masala aliyepata kura 6,494 akifuatiwa naye akipata 5,128.


Wagombea wengine ni Steven Nyoni (1,438), Amandus Chinguile (1,274), Fadhili Liwaka (1,171), Benito Ng’itu (797), Greyson Francis (671), Albert Mnali (763), Issa Mkalinga (466), Mustafa Malibiche (427) na Ali Namnjundu (319).


Mbali ya Chikawe pia manaibu waziri wanne wameangushwa katika kura hizo. Hao ni Mahadhi Juma Maalim (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa), Perera Ame Silima (Mambo ya Ndani), Amos Makala (Maji) na Saning’o ole Telele (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi).


Mahadhi alianguka katika Jimbo la Paje, Zanzibar kwa kupata kura 1,785 huku Jaffar Sanya Jussa ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) Mkoa wa kusini akiibuka mshindi kwa kura 3,368.


Silima aliyepata kura 1,218 katika Jimbo la Chumbuni alibwagwa na mpinzani wake, Ussi Pondeza aliyepata kura 1,952.


Katika Jimbo la Mvomero, Suleiman Murad alishinda kwa kura 13,165 dhidi ya Makalla ambaye alikuwa anatetea jimbo hilo akipata 10,973.


Ole Telele alipata kura 5, 126 huku William ole Nasha akiibuka mshindi kwa kura 23, 563 akifuatiwa na Elias Ngolisa aliyepata 11, 442 na Dk Eliamani Lalkaita 7,135. Matokeo hayo hayakujumlisha kura za matawi matano ambayo Katibu wa CCM Wilaya ya Ngorongoro, Elihudi Shemauya alisema hayawezi kubadili matokeo.


Katika Jimbo la Uzini, Katibu wa Oganizesheni wa CCM, Muhammed Seif Khatib ameshindwa baada ya kupata kura 1,333 huku mpinzani wake Salum Mwinyi Rehani akiibuka kidedea kwa kura 1,521.


Kigogo mwingine wa CCM, Nape Nnauye ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi, ameshinda kura hizo Jimbo la Mtama kwa kura 9,344 dhidi ya mpinzani wake Selemani Methew aliyepata kura 4,766.


Jimbo la Chwaka mbunge wa jimbo hilo kwa miaka 20, Yahya Kassim Issa aliangushwa baada ya kupata kura 1,572 dhidi ya mpinzani wake, Baguwanji Mensuriya Baguwanji aliyepata kura 1,951.


Wakati mawaziri hao wakianguka, Waziri wa Fedha, Saada Mkuya alishinda katika jimbo jipya la Welezo huku Waziri wa Ulinzi, Hussein Mwinyi akishinda katika Jimbo la Kwahani.


Aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM, Masauni Hamad Masauni ameshinda Jimbo la Kikwajuni kwa kura 2,222 dhidi ya mpinzani wake, Mussa Shaali Choum aliyepata kura 461.


Katika Jimbo la Jang’ombe, Ali Hassan Omar ameibuka mshindi kwa kupata kura 879 dhidi ya mpinzani wake Abdullah Hussein Kombo (639).


Aliyekuwa Waziri Kiongozi Zanzibar na waziri wa zamani wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha aliibuka mshindi katika Jimbo la Kijito Upele.


Jimbo la Malindi Abdullah Juma Abdulla alishinda kwa kura 558 dhidi ya mpinzani wake, Kombo Mshenga Zubeir aliyepata kura 241. Jimbo hilo nafasi ya uwakilishi, Mohammed Ahmada Salum alishinda kwa kura 336 na dhidi ya Abdulrahman Hassan (271).


Majimbo mengine
Liwale: Faith Mitambo (7,238), Zainabu Kawawa (3,126).


Ruangwa: Naibu Waziri (Tamisemi), Kassim Majaliwa (11,988), Bakari Nampenya (2,678).


Kilwa Kaskazini: Murtaza Mangungu alishinda kwa kura 7,140.


Kilwa Kusini: Hasanain Dewji ameshinda kwa kura 3,859.


Lindi Mjini: Hassani Kunje (3,428) Mohamedi Ulthali (2,314).


Jimbo la Mchinga: Said Mtanda ameshinda kwa kura 3,101, Riziki Lulida (2,217).


Serengeti: Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Kebwe Steven Kebwe aliibuka mshindi kwa kura 29,268 akiwashinda, Dk James Wanyancha (5,980) na Mabenga Magonera (1,638).


Nyamagana: Aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza, Stanslaus Mabula ameibuka mshindi kwa kura 9,553, Joseph Kahungwa (3,947) na Raphael Shilatu (894) na kufuatiwa na wenzao 17.


Ukerewe: Christopher Nyandiga aliongoza kura 8,077, Gerald Robert (142), Laurent Munyu (197), Emmericiana Mkubulo (242), Bandoma Kabulule (414), Bigambo Mtamwega (477), Dk Elias Missana (648), Hezron Tungaraza (693), Dk Deogratias Makalius (727), John Mkungu (775), Osward Mwizalubi (1,098), Maliki Malupu (1,443), Deogratias Lyato (1,824), Sumbuko Chipanda (2,016) na Magesa Boniphace (2,552).


Morogoro Mjini: Abdulaziz Abood amepata kura 20,094 na Simon Berege (429).


Mikumi: Jonas Nkya alipata kura 947 ameshinda dhidi ya Abdulsalum Sas (544).


Kilombero: Mbunge wa jimbo hilo, Abdul Mteketa alianguka baada ya kushika nafasi ya tatu kwa kupata kura 2,646 nyuma ya Abubakar Assenga aliyepata kura 6,629 na Abdul Liana 3,999.


Mlimba: Godwin Kunamba ameshinda kwa kura 6,233 Dk Fredrick Sagamiko (2,203), Jane Mihanji (2,073).


Gairo: Mbunge wa sasa, Ahmed Shabiby alishinda kwa kura 15,920 akifuatiwa na Omari Awadhi 886.


Morogoro Kusini Mashariki: Omary Mgumba alishinda kwa kura 3,393 akifuatiwa na Jamila Taji (2,914) na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Lucy Nkya (1,710).


Msoma Vijijini: Profesa Sospeter Muhongo aliibuka mshindi kwa kura 30,431 waliofuatia ni Anthony Mtaka (3,457), Evarest Mganga (2,556), Profesa Edson Mjungu (898), Mafuru Mafuru (421), Wits Onyango (392) na Nelson Semba (186).


Butiama: Nimrodi Mkono ameshinda kwa kupata kura 19,366, Chirstopher Siagi (2,457), Samweli Ndengo (745), Jacob Thomas (502), Mwita Wariuba (1,346), Moringe Magige (317), Godfrey Wandiba (303), Joseph Nyamboha (262) na Samweli Gunza (73).


Musoma Mjini: Vedastus Mathayo alishinda kwa kura 6,691 akifuatiwa na Paul Kirigini (1,174), Dk Msuto Chirangi (1,082), Juma Mokili (681), Deus Mnasa (378), Nicodemus Nyamajeje (183), Emmanuel Mwita (155), Felix Mboje (131) na Zerulia Mneno (61).


Kyela: Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe ameshinda kwa kupata kura 15,516, George Mwakalinga (4,905) na Martin Kipija (2,301).


Njombe Kusini: Edward Mwalongo (3,870), Romanus Mayemba (2,153), Daniel Msemwa (1,976), Arnold Mtewele (1,136), Alfred Luvanda (978), Hassan Mkwawa (152), Vitalis Konga (76) na Mariano Nyigu (86).


Makambako: Deo Sanga (7,643) Alimwimike Sahwi (499).
Ludewa: Deo Filikunjombe kabla ya kata tatu alikuwa na kura18,290 akiwaacha Kapteni Jacob Mpangala (205) na Zephania Chaula (770).


Wanging’ombe; Gerson Lwenge kabla ya kata tatu alikuwa na kura 11,322, Thomas Nyimbo (1,871), Yono Kevela (1,819), John Dugange (466), Richard Magenge (417), Abraham Chaula (382), Kennedy Mpumilwa (332), Hoseana Lunogelo (322), Malumbo Mangula (304), Nobchard Msigwa (216), Abel Badi (106) na Eston Ngilangwa (47).


Kiteto: Mjumbe wa NEC, Emmanuel Papian ameshinda kwa kupata kura 40,636 mbunge aliyemaliza muda wake Benedict Ole Nangoro (21,461), Amina Said Mrisho (2,118), Ally Lugendo (287) na Joseph Mwaseba (250).


Bunda Mjini: Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira ameshinda kwa kupata kura 6,429 dhidi ya kura 6,206 alizopata mshindani wake wa karibu, Robert Maboto. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Christopher Sanya alipata kura1,140, Exavery Lugina (846), Simon Odunga (547), Magesa Mugeta (446), Peres Magiri (385) na Brian Bitta (263).


Handeni na Bumbuli
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda pamoja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia January Makamba wameshinda katika mchakato wa kura za maoni katika majimbo ya Handeni na Bumbuli.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: