BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

JINA LA MWANDISHI WA GAZETI LA MWANANCHI LATUMIKA KATIKA UTAPELI


Kwa masikitiko makubwa napenda kuutahadharisha umma wa watanzania juu ya kuibuka kwa mtu tapeli anayejitambulisha kuwa ni DANIEL MJEMA, Mwandishi mwandamizi wa gazeti la Mwananchi.

Novemba mwaka 2013, alijitambulisha hivyo kwa Mwenyekiti wa taifa wa Chadema mhe. Freeman Mbowe na kudai eti mimi nimefiwa na mama yangu.
Kwa mila na desturi zetu, Mheshimiwa Freeman Mbowe pamoja na wabunge kama Esther Bulaya, Grace Kiwelu na wengine walihamasishana na kuchanga rambirambi inayofikia sh900,000.

Mheshimiwa Mbowe na wengine walimpigia simu mtu huyo wakimweleza walitaka kuungana nami (wakiamini ni mimi) kuaga mwili hapo Muhimbili lakini akadai walikuwa wameshaondoka na walikuwa wakielekea Moshi hivyo atumiwe rambirambi hiyo kwa M-Pesa. Alitumiwa fedha hizo.

Lakini Mhe. Grace Kiwelu alitilia mashaka namba hiyo kwa vile namba iliandika jina tofauti na langu lakini kwa bahati mbaya nilikuwa nimepumzika mchana huo.

Nilipokuta missed call yake, nilimpigia kwenye saa 12:00 jioni akaniuliza kama tulikuwa tumefika Moshi. Nilishangaa kwa vile sikuwa nimesafiri kwenda Dar karibu miezi miwili.

Ndipo akashtuka akaniambia "TUMETAPELIWA" na akanieleza hadithi niliyotangulia kuieleza.

Niliwasiliana na Mhe Mbowe akanihakikishia kuwa mtu huyo alijitambulisha kuwa ni Daniel Mjema na alitilia shaka sauti na kumuuliza mbona sauti sio yangu akajitetea ni kwa sababu ya msiba.

Haikuishia hapo, mwaka jana mtu huyo huyo akamtumia sms Dk. Emanuel Nchimbi na kujitambulisha kuwa ni Daniel Mjema wa gazeti la Mwananchi na kwamba nimefiwa na mke wangu.

Dk. Nchimbi alitilia shaka na kumpigia simu managing Editor wangu Denis Msack akiuliza kama nimefiwa na mke wangu naye akamwambia hakuna jambo kama hilo. Dk. Nchimbi akaeleza kuwa Novemba 2013 alimtumia mtu huyo sh200,000 baada ya kujitambulisha kuwa ni Daniel Mjema wa Mwanchi na kwamba nimefiwa na mama yangu jambo ambalo sio kweli. Safari hii alitakiwa tena atumiwe sh200,000.

Dk. Nchimbi alitoa taarifa Polisi na mtego uliandaliwa huko Kibaha Pwani lakini huyo mtu alikuwa smart kwani hakwenda yeye bali alimtuma mwandishi wa hapo Pwani amsaidie kupokea hizo fedha then amtumie kwa M-Pesa.

Nimeeleza kwa kirefu jambo hili kwani mtu huyo ameendelea kutapeli watu katika maeneo mbalimbali hasa mikoa ya kaskazini akibuni njia mbalimbali.

Leo niliitwa kwa Katibu wa CCM mkoa Kilimanjaro na nilipofika hapo nilimkuta akiwa na mtu mwingine akamuuliza unamfahamu huyu(Yaani mimi) yule bwana akasema hanijui na kwamba sio mimi.

Ndipo katibu akaniarifu kuwa kuna mtu ameenda kujitambulisha kwa huyo bwana kuwa yeye ni Daniel Mjema wa gazeti la Mwananchi na kumtapeli sh500,000.

Nilimshauri huyo bwana afungue taarifa Polisi ili mtu huyo aweze kutafutwa.

Ninaomba msambaze taarifa hii ili kuwasaidi raia wema maeneo mbalimbali ya nchi ambao huenda wakatapeliwa leo, kesho au kesho kutwa.

Napenda kutamka kuwa mama yangu mzazi Happyness Mjema na mke wangu mpenzi Tamari Mndeme wako hai kwa mapenzi ya Mungu.

Daniel Mjema
Mwandishi wa Habari
Gazeti la Mwananchi
Kilimanjaro.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: